Zanzibar State Trading Corporation (ZSTC)
Serekali ya Zanzibar

Where Quality Meets Excellence (ZSTC)

Kamati ya Kilimo na Biashara ya Baraza la Wawakilishi yaridhishwa na Utendaji wa ZSTC

Kamati ya Utalii, kilimo na Biashara ya Baraza la Wawakilishi imelipongeza Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) kwa juhudi walizochukua za kuyarudisha baadhi ya maeneo yalioharibiwa kutokana na  shughuli za   uchimbaji wa mchanga  Zilizopelekea eneo hilo kuathirika  na athari za kimazingira.

 

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe,Mtumwa Pea Yussuf katika ziara ya kutembelea na kukagua  Mashamba na Viwanda  vya Shirika hilo Pemba ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukum ya  Kamati hiyo.

 

Aidha  amesema ipo haja Kwa  Shirika kushirikiana na jamii  katika kutunza  Rasilimali zilizopo za Ofisi  ili ziweze kuleta tija kwa  jamii kwa kuongeza uzalishaji hasa kupitia viwanda vya uzalishaji wa mafuta ya Mimea.

 

Akizungumza katika Ziara hiyo Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC)Nd. Soud Saidi Ali amesema kuwa, Shirika litaendelea kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyo tolewa na Kamati hiyo ili kuleta   mabadiliko ndani ya Shiraka.

Katika hatiua nyengine Mkurugenzi Soud amewataka Wafanyakazi wa Shirika hilo kushirikiana na kua na umoja katika kazi ili waweze kuleta maendeleo na kufikia malengo yaliyokusudiwa ndani ya Shirika.

 

Kwa upandewake  Bwana Shamba kutoka Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Nd. Haji Mussa Haji ameeleza kuwa Shirika  litatoa Mashirikiano kwa jamii katika  namna bora ya utumiaji wamashamba hayo iliywawezekutumika kama yalivyokusudiwa na Serikali.  hivyo kupitia Shirika la ZSTC wataendelea kutoa elimu kwa jamii kila inapohitajika alisema.

 

Ziara  hio ya siku moja ya kamati ya Utalii Kilimo na Biashara ya Baraza la  Wawakilishi imetembelea Sehemu mbalimbali ikiwemo  mashamba ya Mikaratusi ya kutengenezea mafuta yaliopo kishindeni Mkoa wa Kaskazini Pemba,Shamba la  mamoja, na kutembelea na kukagua vyungu vya kukamulia  Mafuta  vilivyopo mtakata chake chake Pemba.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Biashara la Taifa ZSTC Nd. Soud Said Ali akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa kamati ya kilimo Biashara na Utalii Mhe Mtumwa Pea Yussuf wakati alipotembelea vyungu vya kukamulia mafuta Mtakata
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Biashara la Taifa ZSTC Nd Soud Said Ali akitoa maelezo kwa kamati ya Biashara kilimo na Utalii ya Baraza la wakilishi wakati walipotembelea Shamba la Mikaratusi Kishindeni